Home » » JINSI YA KUMLAZIMISHA SHAHIDI ALIYEKATAA KUJA MAHAKAMANI AJE MAHAKAMANI

JINSI YA KUMLAZIMISHA SHAHIDI ALIYEKATAA KUJA MAHAKAMANI AJE MAHAKAMANI







Kumekua na dhana ya baadhi ya watu kuogopa Mahakama, hata pindi wanapoombwa kwenda kutoa ushahidi wa matukio walio shuhudia wao hukataa.

Sheria ya mwenendo wa madai [1] imetoa mwongozo wa kumlazimisha shahidi huyo kuja mahakamani kutoa ushahidi katika kesi yako.

Hivyo basi kupitia sheria hiyo utatakiwa kuiomba Mahakama kutoa wito wa shahidi kuhudhuria Mahakamani kwa ajili ya kutoa ushahidi wowote ule unaotakiwa kutolewa kwa ajili ya kujenga kesi yako. Hivyo Mahakama itatoa wito wa shahidi kuhudhuria Mahakamani ( wengi huifahamu kwa jina samansi)

Endapo shahidi atakataa wito wa Mahakama, yani atagoma kuja mahakamani katika tarehe tajwa, Mahakama itatoa tangazo ambalo litabandikwa katika mlango wa nyumba anayoishi au sehemu yoyote ambapo mtu huyu anaweza kuliona tangazo hilo.

Mahakama pia inaweza kutoa amri ya kushikiliwa kwa mali ya shahidi huyo na dalali wa mahakama mpaka atakapo mlipa dalali wa mahakama pamoja na fine au mali zake kuuzwa vile Mahakama itakavyoona inafaa.

Njia nyingine ni kwamba Mahakama imepewa mamlaka yakutoa hati ya kukamatwa kwa shahidi huyo kwa dhamana au bila hata ya dhamana.

Hivyo basi unapaswa kutambua kuwa, pindi unapohitajika kwenda kutoa ushahidi Mahakamani, unapaswa kuitikia wito huo ili kuepukana na usumbufu kama ulivyo ainishwa katika sheria ya mwenendo wa madai


TRINITY COAST  ATTORNEYS,
POBOX 79490, 
DAR ES SALAAM,
5TH FLOOR DARWORTH (BAVARIA) HOUSE,
OFF NYERERE RD., KAMATA TRAFFIC LIGHTS
OPP. NAKUMAT SUPER MARKET






[1] (Chapter 33, order XVI rule 1 mpaka 10)

Jika Anda menyukai Artikel di blog ini, Silahkan klik disini untuk berlangganan gratis via email, dengan begitu Anda akan mendapat kiriman artikel setiap ada artikel yang terbit di Creating Website

0 comments:

Post a Comment

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. BC LEGAL INFORMER - All Rights Reserved
Template Modify by Creating Website
Proudly powered by Blogger